Habari za Simba
Habari za michezo

BAADA YA KUKUNG’UTWA GOLI 5-1 NA YANGA….MBRAZILI SIMBA AVUNJA UKIMYA…KAFUNGUKA HAYA..

admin November 5, 2023 8:09 pm

Akizungumza baada ya timu yake kufungwa magoli 5-1 katika mchezo dhidi ya Yanga, Kocha wa Simba, Roberto Oliveira “Robertinho” amesema kipindi cha pili wachezaji wake walipoteza umakini.

Amesema “Magoli mawili tuliyofungwa kipindi cha pili wachezaji wetu (Simba) walizubaa na kupoteza umakini, walifikiri kuna faulo wenzetu wakaendelea kucheza na wakafunga, nawapongeza wapinzani wetu (Yanga) kwa kushinda ‘Dabi’ na sisi tumepoteza mchezo muhimu.”

Kipigo hicho ni cha kwanza kwa Simba msimu huu katika Ligi Kuu Bara, pia ni cha kwanza kwa Robertinho dhidi ya Yanga tangu akutane na wapinzani hao katika mechi 4 ikiwemo pamoja na zile alizokuwa Vipers.

Kwa matokeo hayo Yanga SC wamefikisha alama 21 na kukwea kileleni mwa Msimamo wakiwa wamecheza Mechi name na kuishusha Azam FC nafasi ya pili wakiwa na Alama 19 wamecheza Mechi tisa huku Simba SC wakibaki nafasi Yao ya tatu wakiwa na Pointi 18 wakiwa wamecheza Mechi Saba.

Rekodi bado itasalia palepale ya Yanga kufungwa goli 5-0, ambayo iliwekwa msimu wa 2013/14, japo leo hii pia ilikaribiwa kuwekwa nyingine kama sio kwa umakini wa manula

FT: SIMBA 1-5 YANGA SC…..MANULA AANZA MSIMU KWA GUNDU….REKODI YAKARIBIWA… WAMELOA….GAMONDI AVUNJA REKODI YA ROBERTINHO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply