Habari za Yanga
Habari za michezo

KUMBE PACOME HAMNA KITU

Staff Desk November 9, 2023 6:26 am

Wakati Wananchi wakifunga wiki iliyopita kwa kishindo cha pekee baada ya kufanikiwa kuitandika Simba mabao 5-1 katika mchezo wa Dabi ya Kariakoo.

Kiungo wa Yanga Pacome Zouzoua aligeuka kuwa mada miongoni mwa wapenda soka kutokana na uwezo mkubwa aliouonesha katika mchezo huo huku kila shabiki akisifu uwezo wake.

Sasa habari ni tofauti kwa mchambuzi wa Michezo kutoka TV3, Alex Ngereza ambae anasema kuwa kiwango cha mchezaji huyo ni cha kawaida na sio sahihi kwa mashabiki kumtukuza kupita kiasi.

Akizungumza Ngereza anasema;

“Binafsi sijaona ubora wa kutisha kwa Pacome Zouzoua ni mchezaji wa kawaida tu na amefanya vizuri sana kwenye zile mechi ambazo Yanga wametawala mpira kwa kiasi kikubwa ila mechi ambazo wamepata ugumu yeye pia ameonyesha kiwango cha kawaida sana mfano mechi dhidi ya Namungo na mechi dhidi ya Ihefu siku zote mchezaji bora anafanya vizuri bila kujali ugumu wa mpinzani ila yeye bado anachagua mechi”

KAGERA SUGAR WAJA NA MKAKATI MPYA LIGI KUU HUKO YANGA UNAAMBIWA UBABE UBABE TU

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply