Habari za Simba leo
Habari za michezo

KUELEKEA MECHI NA ASEC MIMOSAS….MASTAA NA MSHABIKI SIMBA WAPEWA UJUMBE HUU MZITO…

admin November 17, 2023 5:17 pm

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally amewataka mashabiki kusahau yaliyopita na kujitokeza uwanjani.

Ahmed ameyasema hayo leo alipokuwa kwenye mkutano na wanahabari akizindua rasmi kampeni yao ya kuelekea mchezo wao wa kwanza wa hatua ya Makundi Kimataifa dhidi ya ASEC Mimosas.

“Safari hii tunakwenda kuwashangaza watu, tutaujaza uwanja wa Mkapa. Niwambie Wanasimba kama una hasira uje nazo furaha utaikuta uwanjani.”

“Kauli mbiu yetu ya mchezo dhidi ya ASEC Mimosas ni Twendeni Kinyama, Mashabiki Bomba,” alisema Ahmed Ally.

Katika hatua nyingine, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Klanbu ya Simba, Ahmed Ally amesema kuwa kejeli licha ya kufungwa na watani zao bao 5-1 kisha sare na Namungo FC kwa bao 1-1, bado wana imani na wachezaji wao.

Ahmed amesema hayo leo Novemba 16, 2023 wakati akizindua kampenzi ya hamasa kuelekea mchezo wa hatua ya makundi wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya ASEC Mimosas utakaopigwa Novemba 25, 2023 katika Dimba la Mkapa.

“Sisi tuko bega kwa bega na wao, lakini tuwakumbushe kwamba yale yote yaliyopita wanapaswa waachane nayo, wasiingie uwanjani wakijihisi wakosefu au wanyonge kwamba tumewapelekea matatizo, waingie uwanjani kifua mbele kuipigania klabu yetu.

“Tuna imani na wachezaji wetu kwamba wanaweza kufanya makubwa na wameshathibitisha hilo, Novemba 25 wakaendeleze hayo makubwa. Tumeteleza hatujaanguka,” amesema Ahmed Ally.

UONGOZI SIMBA WAWAANGUKIA WACHEZAJI, ISHU IKO HIVI KUHUSU BANGO LA 5G LA YANGA….SIMBA WAAMUA KUCHUKUA HATUA HIZI MAPEMAA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply