Habari za Yanga
Habari za michezo

KWA KUNDI HILI LA YANGA KWELI MBOGA MOTO UGALI MOTO

Staff Desk December 4, 2023 4:51 pm

Mechi mbili zijazo kwenye kundi (D) zitatoa mwanga utakaoonesha timu zipi zina nafasi kubwa ya kutinga robo fainali CAF champions league 23/24.

Yanga walianza ratiba yao kwa mtego kwenye kundi (D). CR Belouizdad ugenini, Al-Ahly nyumbani. Point 1 sio mbaya wala nzuri kwa ratiba hiyo.

Turning point ya Yanga wakijipanga vyema huenda ikaanzia hapa :

Medeama vs Yanga

Yanga vs Medeama

Al-Ahly vs CR Belouizdad

CR Belouizdad vs Al-Ahly

◉ Yanga anahitaji kushinda dhidi ya Medeama home & Away ili kufikisha points (7). Wakati huo yeye akifikisha points (7), Waarabu ambao ndio wapinzani wagumu watakuwa wanauana wao kwa wao.

◉ Baada ya mechi hizo mbilimbili kupita, Yanga atabaki na mechi (1) dhidi ya CR Belouizdad nyumbani kwa Mkapa.

Akichukua points (3) kwa CR Belouizdad na kufikisha (10) taa ya kijani Kuelekea Robo

fainali CAF champions league itawaka

◉ Kinyume chake, hesabu zitakuwa ngumu sana kutinga robo fainali. Yote yako mikononi mwa Yanga kwani bado kuna points (12) za kugombea mpaka sasa.

So far, hata Wydad Athletic ambaye hana point katika michezo (2) ananafasi ya kutinga robo fainali. Bado ni asubuhi.

SIO SIMBA, YANGA MAMBO NI MAGUMU STORI KAMILI IKO HIVI BAADA YA KUYEYUSHA DK 540 ZA CAF BILA LOLOTE…BENCHIKHA KUWASHUSHIA DAWA HII SIMBA..

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply