Habari za Simba
Habari za michezo

SIMBA IMEBADILIKA KILA KITU…. TATIZO BADO LIKO HAPA

Staff Desk December 7, 2023 1:26 pm

Mchambuzi wa soka Bongo George Ambangile amesema Simba SC imebadilika kutoka ile iliyokuwa inaruhusu sana magoli na kilichobaki ni kupachika magoli kwenye nyavu.

Ambangile ametoa maoni hayo alipokuwa akiichambua mechi ya Simba dhidi ya Jwaneng Galaxy ambayo iliisha kwa sare ya 0-0.

“Simba walikabia juu, Saido, Kibu na Baleka walianza kukaba vizuri kuanzia juu lakini sio hao tu viungo wakabaji Kanoute na Ngoma walisogea, vilevile mabeki wa pembeni walisogea juu na kuwafanya Jwaneng waanze kupiga mipira mirefu.

“Nimeona Simba imebadilika na hii ni meseji nadhani kutoka kwa Kocha Benchikha kwamba usipojitoa kukaba unapoteza namba,” alisema Ambangile.

MTEGO WA CHAMA DHIDI YA WYDAD UMEKAA HIVI CHAMA NAE AONYESHWA MLANGO WA KUTOKEA MSIMBAZI….. ISHU IKO HIVI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply