Habari za michezo
SIMBA KUWATUMIA KAGERA SUGAR KAMA DARAJA LIGI KUU, UONGOZI WAFUNGUKA HAYA
Staff Desk
December 13, 2023
1:53 pm
Ahmed Ally ambaye ni Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, amesema wanahitaji ‘ufufuo’ kupitia Kagera Sugar Ijumaa hii katika mechi ya Ligi Kuu ya NBC.
Ahmed ametoa kauli hiyo mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa Simba Queens dhidi ya JKT Queens katika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar na Simba kuibuka na ushindi wa penalti 5-4.
“Tunahitaji ufufuo kupitia Kagera Sugar, tukishamalizana na Kagera tutahamia kwa Wydad AC mchezo ambao hakuna mwanaSimba atabaki nyumbani, wote twendeni Benjamini Mkapa kuhakikisha tunamfanya vibaya Wydad,” alisema Ahmed.
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.