Habari za Michezo leo
Habari za michezo

“KELVIN JOHN HASTAHILI KUJIITA MBAPPE….KWANZA ANADHARAU NA NIDHAMU MBOVU”….

admin January 1, 2024 11:58 pm

WAKATI wadau wengi wakihoji kukosekana kwa jina la mshabuliaji wa KRC Genk, Kelvin John kwenye kikosi cha timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ kinachoenda kushiriki fainali za mataifa ya Afrika (Afcon) kocha mkuu wa timu hiyo Adel Amrouche amefunguka sababu.

Amrouche amefunguka hayo saa chache kabla ya kuondoka kwenda Misri kwa ajili ya kambi ya timu ya taifa alisema nidhamu mbovu aliyonayo ndiyo imemuengua kikosini.

Alisema ni mchezaji mzuri endapo atabadilika na kuamua kuwekeza nguvu kiwanjani huku akiupa mchezo huo heshima kwa kuwa na nidhamu bora kiwanjani na nje ya uwanja.

“Sijaita kikosi kwasababu ya mtu fulani hiki ni kwa ajili ya Tanzania, hivyo Tanzania kwanza, natambua uwezo wa mchezaji huyo ni mzuri natakiwa kumlinda na kukuza uwezo wake nitafanya hivyo endapo atabadilika;

“Hapaswi kulinganishwa na Mbappe, Mbappe ni mchezaji mkubwa ni nahodha wa timu yake ya taifa amekuwa akilipambania taifa lake pale Ufaransa, huyo Kelvin anatakiwa kubadilika na kupambania nafasi ya kucheza kikosi cha kwanza siwezi kuacha wachezaji ambao wanacheza nikamchukua mchezaji anatokea benchi na ananidhamu mbovu,” alisema

USAJILI MPYA WAANZA NA BALAA ZITO SIMBA…PHIRI AKIANZA ‘KUJISHTUKIA’ MDOGO MDOGO… GAMONDI – OKRAH..? USAJILI SAFI LAKINI….ISHU YA CHAMA SIMBA IKO HIVI…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply