Moses Phiri
Habari za michezo

WAKATI JAMBO LA CHAMA LIKIWA TETE….BENCHIKHA AMPIGA MKWARA MZITO PHIRI…

admin January 8, 2024 8:18 pm

Kocha Mkuu wa Simba SC, Abdelhak Benchikha ametoa onyo kwa mastaa wa klabu hiyo, ambao wamepewa nafasi nyingi kupitia michuano ya Mapinduzi ambao walikuwa hawapati nafasi ya kucheza kuitumia vyema ili kumshawishi kuweza kuingia katika kikosi chake akiwemo nyota Moses Phiri.

Phiri tangu kuanza kwa msimu huu amekuwa hapati nafasi ya kutosha huku kwenye michuano ya Mapinduzi inayoendelea kutimua vumbi visiwani Zanzibar amekuwa akipewa nafasi mara kwa mara na amefanikiwa kufunga bao moja.

Kocha Benchikha amesema: “Kwa wale wachezaji wote ambao walikuwa hawapati nafasi ya kucheza mara kwa mara, tumejaribu kuwapa nafasi ya kutosha ili waweze kuonyesha mabadiliko na kulishawishi benchi la ufundi.

“Kwa hali nyingine, hii ni kawaida lakini kwa wachezaji wanatakiwa kupambana ili kuleta ushindani wa namba na hapo itakuwa ni faida ya timu kwa kuwa maendeleo yatakuwa yanapatikana kupitia wachezaji kujituma, ili walinde nafasi zao.

Gamondi aandaa mfumo mpya Young Africans
“Sisi kama Simba SC na ukubwa wa hii timu, hatutaki kuona mchezaji anajihajikishia namba kwani tunataka ushindani na ndio maana wamepewa nafasi kupitia hii michuano ili waweze kulishawishi benchi la ufundi” amesema kocha huyo.

WAKATI YANGA WAKIIKIMBIA SIMBA JANA…SINGIDA WAWAHI SITI YA MBELE KABISA… KUHUSU ISHU YA KUWAACHA KONKONI , GIFT….MABOSI YANGA WAPASUA VICHWA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply