Habari za Yanga SC
Habari za michezo

WAKATI WATU WAKIDHANI GSM NDIO KILA KITU…ENG HERSI AMTAJA ALIYEIPA MAFANIKIO YANGA…

admin February 29, 2024 8:35 pm

Rais wa Klabu ya Young Africans, Eng. Hersi Ally Said amesema kuwa, mtu aliyeko nyuma ya mafanikio ya Klabu hiyo ni Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.

Hersi amesema hayo wakati akihojiwa na Kituo cha Televisheni cha Al Ahly mjini Cairo, nchini Misri ambako timu yake imekwenda kwa ajili ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika.

“Chachu ya mafanikio ya mpira wetu Tanzania ni Rais wetu Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wetu amekuwa na mchango mkubwa sana kwenye soka la nchi yetu.

Taifa Stars kufuzu kwenda kwenye fainali za AFCON 2023 nchini Ivory Coast ni moja katika mafanikio yake.

Kufaulu kwa UMOJA BID katika kuandaa AFCON 2027 ni sehemu kubwa ya jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan.

Aidha mchango wake mkubwa katika kujenga Hamasa kupitia “GOLI LA MAMA” umeifikisha Young Africans katika fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika 2022/23 na sasa Young Africans kufuzu kwenda robo fainali ya Klabu bingwa barani Afrika.

Asante Sana Mama” Amesema Rais wa Young Africans Eng.Hersi Ally Said kwenye Kituo cha Televisheni cha @alahlytv Cairo, Egypt

KUHUSU UBINGWA WA LIGI KUU….KOCHA AZAM FC ANYOOSHA MIKONO KWA YANGA… UANZE MWEZI MARCH KWA KUVUNA KIBUNDA CHA MERIDIANBET CASINO NA SLOT HII MPYA..

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply