UNAIKUMBUKA Mamelodi Sundowns ya Pitso Mosimane? huenda huko mbali, je hii Mamelodi ya Rulani Mokwena? kwenye ubora ule na kiwango kile nyuma yake alikuwepo Kocha Steve Komphela ambaye jina lake lipo kwenye meza ya Mnyama Simba likiendelea kujadiliwa.
Inaelezwa kwamba Steve Komphela ambaye kwa sasa anafundisha klabu ya Golden Arrows inayoshiriki Ligi kuu ya Afrika Kusini, anatajwa kuwa Mrithi wa nafasi ya Benchika ambayo ilikuwa ikikaimiwa na Juma Mgunda.
Simba na Coastal Union wamemalizana na Kocha Mgunda ambaye, atajiunga nao kama kocha mkuu ili kukinoa kikosi hicho cha Wagosi wa Kaya kwenye mashindano ya kimataifa ya Kombe la Shirikisho, ratiba inaonesha Agosti michuano hiyo itaanza kwa timu zinazoanzia hatua ya awali kabisa.
CV YA KOCHA HUYU USIPIME
Wasifu wa Kocha huyu ambaye amefundisha kama kocha mkuu wa Mamelodi na kocha msaidizi chini ya makocha wakubwa kama Pitso na Mokwena, nadhani imewavutia zaidi Simba hadi kufikia hatua ya kumtaka haraka. Ni muumini wa mfumo wa 4-4-2 double 6.
2023/24: Amefundisha kama kocha Mkuu Golden Arrows.
2011/12, Timu ya Taifa ya Afrika Kusini, Kocha Msaidizi.
Pia kocha huyo, kwa wakati tofati amewahi kuwa kocha Mkuu wa vilabu kama, FS Stars, Platnum Stars, Afrika ya Kusini chini ya umri wa miaka 20, Dynamos FC na Maning Rangers.