- Habari za michezo
- Habari za Simba
- Habari za Simba Leo
- Michezo
- Michezo Bongo
- Michezo Soka la Bongo
- news
- Simba SC
Simba ya Kocha Fadlu Davids imekuwa ikitumia mifumo ya 4-2-3-1 na 4-4-2 ambayo imeiwezesha wachezaji kunyumbulika, kufanya majukumu mengi uwanjani na hilo wamekiri kwa nyakati tofauti.
Pamoja na maigizo mapya Simba kama Leonel Ateba, Joshua Mutale na Jean Charles Ahoua, inahitaji muunganiko na uzoefu utakaofanya kila mechi iwe nyepesi kwao.
Moja ya mambo muhimu yanayochangia mafanikio ya timu yoyote ni maandalizi thabiti na nidhamu. Benchi la ufundi la Simba linafanya kazi kubwa kuandaa wachezaji wao kimwili na kiakili ili wawe na nguvu na utayari wa kucheza mechi nyingi bila kuchoka.
Simba inafaidika na uongozi bora ambao unahakikisha timu inapata mahitaji muhimu, ikiwa ni pamoja na usajili, mafunzo na mazingira mazuri ya kazi kwa wachezaji na benchi la ufundi.