Bao jingine la Yanga katika mechi hiyo iliyopigwa Juni 25 mwaka jana lilifungwa na Pacome Zouzoua ambaye alikuwa jukwaani na baadhi ya nyota wengine katika mechi hiyo ya jana.
Mara baada ya pambano hilo la saba kwa Simba na Yanga kukutana Zanzibar na la kwanza kwa Ligi Kuu Bara msimu huu, timu hizo zitarudi jijini Dar es Salaam kabla ya kujiandaa na mechi zijazo za Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho.
Yanga itakuwa ya kwanza kucheza keshokutwa Alhamisi ugenini kukabiliana na Singida Black Stars kisha Machi 8 itaumana na Polisi Tanzania katika pambano la 32 Bora la Kombe la Shirikisho (FA) na Machi 12 itaumana na Tanzania Prisons pia ugenini jijini Mbeya na Machi 15 itavaana na Azam.
Kwa upande wa Simba yenyewe itaanza Kombe la Shirikisho Machi 7 dhidi ya B19 FC na Machi 11 itaifuata Singida BS kwa mechi ya Ligi Kuu itakayopigwa ugenini kabla ya kujisogeza mjini Tabora Machi 14 kumalizana na Watoza Ushuru wa TRA United kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.
YANGA: Diarra, Mwenda, Tshabalala, Bacca, Job, Damaro, Maxi, Duke, Depu, Mudathir na Dube
SIMBA: Kassali, Kapombe, Kibabage, Toure, Rushine, Kagoma, Guaye, Kante, Oura, Chama na Inno