Metacha Apewa Mitatu Singida Black Stars
BAADA ya golikipa wa Singida Black Stars, Metacha Mnata kumaliza mkataba wake msimu ulioisha wa 2025-2026, imeelezwa kwamba uongozi wa timu hiyo umempatia mwingine wa miaka mitatu.
“Ukitaja magolikipa wazawa wanaofanya vizuri, huwezi kuliacha nyuma jina la Metacha, ana uzoefu mkubwa wa michuano ya kimataifa, kulingana na majukumu ya msimu ujao tumeona huduma yake ni muhimu,” kilisema chanzo hicho na kuongeza;
“Kabla ya msimu mpya kuanza Agosti 14, mbele yetu tuna michuano ya Kombe la Cecafa Kagame 2026, hivyo lazima tuwe na wachezaji kama Metacha katika timu.”
Singida Black Stars baada ya kumaliza nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC, itashiriki Kombe la Shirikisho Afrika kwa msimu wa pili mfululizo baada ya 2025-2026 kuishia makundi.
Singida ni miongoni mwa wawakilishi wa Tanzania katika mashi ndano ya Kagame, timu hiyo inakwenda kushiriki ikiwa bingwa mtetezi, ikiambana na Simba ambayo ni bingwa wa kihistoria ikishinda mataji sita. Pia kuna KVZ ya Zanzibar.