Uncategorized

OBREY CHIRWA ATAKA KUREJEA YANGA

admin May 30, 2019 6:44 am


IMEELEZWA Kuwa baada ya mshambuliaji wa Azam FC, Obrey Chirwa kuigomea klabu hiyo kuongeza mkataba mpya ndani ya klabu hiyo ameanza mazungumzo na kikosi cha Yanga ili kujiunga nao msimu ujao.

Taarifa kutokana ndani ya Yanga zimeeleza kuwa Chirwa amekuwa akiwasiliana na viongozi wake wa zamani ili kuona namna gani anaweza kurejea tena kwenye kikosi chake cha zamani.

“Amekuwa akifanya mawasiliano na viongozi wa juu ili kurejea hapa Jangwani, unajua Chirwa kuna vitu anavikosa kule alipo ndio maana anadengua kuongeza mkataba,” kilieleza chanzo.

Akizungumza juu ya hatma ya Chirwa na Saleh Jembe, mratibu wa Azam FC, Philip Alando amesema kuwa wamekubaliana kusubiri mkataba wake uishe ili wakae mezani ikishindikana watamuacha.

“Chirwa ni mchezaji na anajielewa hivyo mkataba wake ukikamilika tutakaa naye mezani maana tulikuwa tunasubiri ligi iishe ndipo tujadili, kama atahitaji kuondoka itakuwa ni uamuzi wake,” amesema.

Kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera aligoma kuzungumzia suala la kumrejesha Chirwa kwani awali alipotaka kujiunga na Yanga alimkataa waziwazi.

Walcot asajiliwa Yanga. YANGA WAIPANGIA KIKOSI CHA MAUAJI AZAM FC

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply