Uncategorized

LIPULI: HATUNA MKWANJA ILA KOMBE TUNASEPA NALO

admin May 31, 2019 10:24 am

KOCHA wa timu ya Lipuli, Seleman Matola amesema kuwa bado hali ndani ya kikosi kwa upande wa uchumi haijakaa sawa ila amewajenga kisaikolojia wachezaji wake kubeba kombe la FA mbele ya Azam FC Juni Mosi.

Akizungumza na Saleh Jembe, Matola amesema kuwa tatizo la ukata limekuwa sugu ukichanganya na ugumu wa ratiba kwake ila hilo ameweka pembeni na kulipigia hesabu kombe.

“Kwa sasa kikosi kina hali mbaya kiuchumi najua kabisa sina hela ila nimewajenga wachezaji wangu kupambana na tutapata matokeo kwenye mchezo wetu uwanja wa Ilulu.

“Ushindani ni mkubwa na timu ninayocheza nayo ipo vizuri kwenye kila idara ila hilo halinipi taabu, nimezungumza kuhusu kubwana na ratiba sasa ninakwenda kuonyesha kazi yenyewe uwanjani mpaka nibebe kombe,” amesema Matola.

AZAM FC: TUPO TAYARI KUWA WA KIMATAIFA WACHEZAJI WANAOTEMWA YANGA HAWA HAPA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply