Uncategorized

Hakuna uhakika wa Zana

admin June 11, 2019 11:28 am

Kandanda inatambua kuwa kuna uwezekano mkubwa sana beki wa kulia wa Simba Sc aliyekuja kuziba nafasi ya Shomari Kapombe, hatarudi tena.

Zana Coulibaly aliaminika kuwa ni mbadala wa Shomari Kapombe ambaye aliumia akiwa na kikosi cha Taifa Stars, ameshindwa kuwashawishi Simba ili aongezewe mkataba. Tetesi hizi zimetua katika Meza ya Uhamisho ya Kandanda baada ya Simba kuanza kutoa taarifa za usajili wao.

Beki huyu mwenye mbwembwe nyingi nje na ndani ya uwanja lakini pia msaurifu wa majukumu yake awepo uwanjani, kwa kiwango fulani ameisaidia sana Simba katika kutengeneza/kutoa pasi za mwisho za goli.

Ingawa uongozi wa Simba umekataa kuhusu tetesi za Zana kuachwa ni za uzushi, lakini ni wazi Zana kubaki Simba ananafasi ndogo sana.

Kandanda inaendelea kufuatilia kujua pia wachezaji gani wanaondoka, na nani pia atachukua nafasi ya Zana kwakuwa hata Kapombe pia bado hajapona.

The post Hakuna uhakika wa Zana appeared first on Kandanda.

LIPULI YAMCHUNIA MATOLA, KAMBI YAO YAVUNJWA KIMAAJABU AISHI MANULA APIGWA PINI RASMI MIAKA MITATU

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply