Uncategorized

YANGA YAKAMILISHA ASILIMIA 90 YA USAJILI WA ZAHERA,

admin June 17, 2019 12:23 pm


UONGOZI wa Yanga umesema kuwa kwa umekamilisha mchakato wa usajili wa wachezaji wake kwa asilimia 90 kutokana na maagizo ya kocha Mkuu, Mwinyi Zahera.

Mwenyekiti wa Yanga, Dk. Mshindo Msolla amesema kuwa usajili wote walioufanya umetegema ripoti ya kocha hivyo wana imani wataleta ushindani kwenye michuano ya kimataifa.

“Kazi ya usajili tumeifanya kwa kuzingatia matakwa ya kocha, imani yetu tutafanya kweli kwenye michuano ya ndani na ya kimataifa,” amesema Msolla.

Mashine mpya ambazo zimesajiliwa ni pamoja na Patrick Sibomana, Lamine Moro, Issa Bigirimana, Maybin Kalego, Mustapha Suleiman, Juma Balinya, Sadney Urikhob na Abdulaziz Makame.

PASIPOTI YAMZUIA AIYEE KWENDA SWEDEN KAZI IMEANZA AZAM FC, YAMCHOMOA WINGA MATATA MBEYA CITY

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply