Uncategorized

BARUA YACHELEWESHA DILI LA MGHANA SIMBA

admin June 30, 2019 11:05 am


WAKATI mkataba wa nyota wa Simba, Nicholas Gyan raia wa Ghana ukikoma mwezi ujao, imethibitika kuwa beki huyo anasubiri barua tu ili aweke wazi timu anayokwenda.

Meneja wa nyota huyo, Juma Ndambi alisema kinachowakwamisha kwa sasa ni barua kutoka Simba na wamekuwa kimya bila kueleza lolote kuhusiana na mkataba wa mchezaji huyo.

Meneja huyo aliongeza kuwa mpaka sasa wamepokea ofa kutoka klabu mbalimbali na wana- tarajia kusaini mkataba wa awali huku wakiendelea kuisikilizia Simba.

“Simba wapo kimya hawasemi lolote kuhusu mchezaji wangu na kwa sasa tunafuatilia barua tu ambayo tukipata tutaendelea na taratibu nyingine.

“Awali nilisema kuwa kuna timu ambazo zilionyesha nia ya kutaka kumsajili moja ya nje na nyingine za hapa ndani na tunasaini mkataba wa awali huku tukisubiri majibu ya Simba ingawa kwa sasa wakitupa barua ndiyo itakuwa vizuri zaidi,” alisema Ndambi ingawa habari zinamhusisha mchezaji huyo na Kaizer Chief ya Afrika Kusini.

KIUNGO MPYA YANGA ATIBU USAJILI MANULA BOMU KWETU, HUKU WENYE MPIRA WAO WANAMUONA YUKO VIZURI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply