Uncategorized

WAWA: NINAONDOKA BONGO

admin June 4, 2019 12:29 am

BEKI kisiki wa Simba mwenye mwili uliojengeka kimazoezi Pascal Wawa amesema kuwa kwa sasa anatarajia kuondoka bongo muda wowote kuelekea nchini Ivory Coast kwa ajili ya mapumziko mafupi.

Akizungumza na Saleh Jembe, Wawa amesema kuwa baada ya kutwaa ubingwa ndani ya kikosi cha Simba ni muda mwafaka kwake kusepa kwenda nyumbani kupumzika ili kujiandaa kwa msimu ujao.

“Nashukuru, kwa kushirikiana na wenzangu tumebeba ubingwa hilo lilikuwa ni jambo kubwa na la msingi, kilichobaki kwa sasa ni kuondoka kurejea nyumbani kuiona familia yangu.

“Sitakaa sana hapa bongo inanibidi niondoke kwa kuwa nilikuwa ninamajukumu namalizia ila kwa sasa nitaondoka kwa ajili ya kupumzika,” amesema Wawa ambaye amecheza jumla ya michezo 21 ndani ya Simba.

MLINZI WA SHULE ALIYEMUUA MWANAFUNZI AHUKUMIWA KIFO KOCHA JULIO: YANGA NI TISHIO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply