LEO wawakilishi wa Tanzania kwenye michuano ya Kagame inayofanyika nchini Rwanda watakuwa kazini kupeperusha Bendera.
KMC watakuwa wa kwanza kurusha kete yao leo majira ya saa 7:00 mchana watamenyana na Atlabara, huu pia ni mchezo wa kwanza kwa kocha mpya Jackson Mayanja.
Azam FC ambao ni mabingwa watetezi watarusha kete yao majira ya saa 9:00 alasiri watamenyana na Mukura, huu utakuwa ni mchezo wa kwanza kwa kocha wao mpya Ettiene Ndayiragije.







