Uncategorized

TAMBWE AMPA MAAGIZO ZAHERA

admin July 14, 2019 9:03 pm


Amis Tambwe amepaza sauti kutoka Burundi hadi Tanzania akimtaka Kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera amrudishie kitambaa cha unahodha beki Kelvin Yondani.

Yondani alipewa kitambaa cha unahodha kwenye mechi za maandalizi za msimu uliopita baada ya beki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ kustaafu lakini baadaye Yondani alivuliwa kwa madai ya utovu wa nidhamu.

“Tusubiri tuone kama Zahera atakubali ushauri kuhusu hili la kumrudishia Yondani kitambaa japokuwa nafahamu ana misimamo yake na kila mtu anaijua, hakuna mchezaji anayestahili kuwa nahodha zaidi ya Yondani.”

“Kwanza kabisa ni mchezaji mzoefu lakini pia kwa sasa ndiye mchezaji mkongwe katika kikosi hicho kuliko wengine wote na ana heshimika na kila mchezaji kutokana na uwezo wake uwanjani.”

KAGERE AKIMBILIA GYM FAINALI YA KUNDI LA TANZANIA AFCON ITANOGA KINOMA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply