Uncategorized
HAYA NDIYO MAKOMBE ANAYOYATAKA NYOTA MPYA WA BARCELONA ANTONIE GRIEZMANN
ANTONIE Griezmann, nyota mpya wa Barcelona ambaye amesaini kandarasi ya miaka mitano amesema kuwa hesabu zake kubwa ndani ya kikosi hicho ni kubeba makombe yakutosha.
Griezmann amejiunga na Barcelona akitokea Atletico Madrid kwa dau la pauni milioni 108.
“Nafikiria kuwa nimekuja hapa kupata upinzani mpya na nitafanya mambo makubwa sana kuhakikisha ninakuwa kwenye kiwango kikubwa.
“La Liga, Copa del Rey na Ligi ya Mabingwa Ulaya ndiyo yanayotakiwa na timu hii na mimi ninaamini kuwa nitayatwaa,” amesema.

Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.