Uncategorized

LEICESTER CITY YAZIKAZIA MANCHESTER CITY NA UNITED KWA BEKI WAO

admin July 17, 2019 10:01 pm


BRENDAN Rodgers bosi wa Leicester City amethibitisha kwamba tayari timu yake imeachana na ofa za timu mbili ambazo zilikuwa zinahitaji huduma ya beki wao wa kati Harry Maguire.

Licha ya ofa hizo mbili kwa nyota huyo wa Taifa la England ambaye alikuwa sehemu ya kikosi kilichocheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Scunthorpe siku ya Jumanne na waliibuka na ushindi wa bao 1-0.
Maguire amezivutia timu nyingi kubwa ikiwa ni pamoja na Manchester United na Manchester City ambao walikuwa wanahitaji huduma yake kwa dau la thamani ya pauni milioni 90.
“Harry ni mchezaji wa thamani ya juu na ana uwezo mkubwa inakuwa ni ngumu kwa sasa timu kukubali kumuuza, zipo timu ambazo zinamhitaji ila bado tunaona ni kijana mzuri kwetu na ana uhakika wa kupata namba kama ambavyo alifanya kwenye dakika 45 alizocheza,” amesema.

HAJI MANARA AMZUNGUMZIA JACKLINE WOLPER REAL MADRID KUUZA NYOTA WATANO KUMPATA NYOTA WA MANCHESTER UNITED

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply