Uncategorized
MASHABIKI WANAAMINI DEMBELE ATAPELEKWA NA GRIEZMANN LIVERPOOL
MASHABIKI wa Liverpool wamebeba imani kwamba kusajiliwa kwa Antonie Griezmann kutawapa neema ya kumpata nyota wa kikosi cha Barcelona, Ousmane Dembele.
Barcelona waliweka mezani kitita cha pauni milioni 108 na kumsajili winga, Griezmann ingawa jambo hilo bado linapingwa na klabu yake ya Atletico Madrid.
Mashabiki wa Livepool wanaamini kuwa kitendo cha nyota huyo kutua Barcelona kitampa wakati mgumu wa kupata namba Dembele ndani ya kikosi hicho hivyo njia nyepesi ni kutimkia Liverpool ambao inaelezwa kuwa wanahitaji saini yake.

Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.