TAYARI nyota wanne wa Simba ambao walikuwa wamekwama kukwea pipa na kujiunga na timu nchini Afrika Kusini wameshatia timu na leo wamefanya mazoezi na wachezaji wengine.
Wachezaji hao ambao ni Meddie Kagere, Deo Kanda, Francis Kahata na Sharaf Shiboub walikwama kuondoka na timu Jumatatu kutokana na kushughulikia paspoti.
Simba imeweka kambi ya muda wa wiki mbili nchini Afrika Kusini kwa ajili ya maadalizi ya msimu ujao.






