Uncategorized

KASSIM KHAMIS, IDDY SULEIMAN WAMPA WAKATI MGUMU NYOTA AZAM FC

admin July 21, 2019 12:12 am

KUSAJILIWA kwa nyota wa Mbeya City FC, Iddy Suleiman, Kassim Khamis kutoka Kagera Sugar kumefanya nafasi ya mshambuliaji Mbaraka Yusuph kuwa finyu hali inayowafanya mabosi hao kufikikria kumtoa kwa mkopo Mbaraka Yusuph.


Yusuph alitolewa kwa mkopo Namungo FC na tayari amemaliza mkataba wake kwa sasa amerejea Bongo akiisubiri timu irejee kutoka Rwanda ambao inashiriki michuano ya Kagame na leo inacheza fainali.

Habari zinaeleza kuwa kwa sasa mabosi wa Azam FC wanafikiria kumtoa kwa mkopo kumrejesha Kagera Sugar mchezaji huyo ili alinde kipaji chake jambo ambalo Yusuph kaligomea.

“Mimi ni mchezaji wa Azam kwa kuwa nimemaliza mkataba wa kuitumikia Namungo, ishu ya kutolewa kwa mkopo tena sijaipata kwa sasa ninachojua msimu ujao nitakuwa ndani ya Azam FC,” amesema. 
YANGA MPYA YANGA ATAJA SIKU YA KUTUA BONGO KAZI IMEANZA MTIBWA SUGAR, WAINASA SAINI YA NYOTA WA TIMU YA TAIFA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply