Uncategorized

NYOTA STARS AENGULIWA MOJAKWAMOJA KAMBINI

admin July 24, 2019 9:36 pm

MUDHATHIR Yahya sasa hatakuwa sehemu ya kikosi cha timu ya Taifa kutokana na kusumbuliwa na tatizo la kifundo cha mguu.

Timu ya Taifa ya Tanzania ipo kambini kwa ajili ya maandalizi ya michuano ya Chan na mchezo wake wa kwanza ni Julai 28 dhidi ya Kenya Uwanja wa Taifa.

Akizungumza na Saleh Jembe, Kocha Msaidizi wa Taifa Stars, Juma Mgunda amesema kuwa wameamua kumpa mapumziko moja kwa moja mchezaji huyo ili apate matibabu.

“Mudhathiri hatakuwa sehemu ya kikosi chetu kwa kuwa hali yake haipo imara, ataendelea kupata matibabu ili kutengamaa na kureea kwenye ubora wake,” amesema.

Mudhathiri alipata maumivu hayo kwenye timu ya Taifa ya Tanzania wakati wa michuano ya Afcon nchini Misri hakushiriki pia michuano ya Kagame iliyofanyika nchini Rwanda.

MTIBWA SUGAR YAMALIZANA NA MAJEMBE MANNE FASTA RUVU SHOOTING: TUNAKIWASHA KWA KASI MSIMU UJAO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply