Mwambusi
Uncategorized

MBEYA CITY: TUNAMALIZIA SUALA LA USAJILI

admin July 25, 2019 3:31 am


JUMA Mwambusi, Kocha Mkuu wa Mbeya City amesema kuwa kwa sasa wanakamilisha utaratibu wa mwisho kusajili wachezaji wapya kabla ya dirisha la usjili kufungwa.

Mwambusi amejiunga na timu ya Mbeya City baada ya kupigwa chini na Azam FC msimu uliopita kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kuwa na matokeo mabovu.

“Kwa sasa bado tunakamilisha suala la usajili kwa kuwa ni lala salama, utaratibu ukikamilika ndipo tutakuwa huru kuendelea kujipanga kwa ajili ya msimu ujao.

“tunaamini ushindani utakuwa mkubwa ila tupo tayari kwani kila kitu kinakwenda sawa,” amesema.

Dirisha la usajili linatarajiwa kufungwa Agosti 31 na Shirikisho la Soka Tanzania limesema kuwa hakutakuwa na muda wa kuongeza.

AZAM FC YAWAITA MASHABIKI KUIPASAPOTI KIMATAIFA ISHU YA MDHAMINI MKUU WALIGI KUU BARA IMEFIKA HAPA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply