Uncategorized

MOHAMED SALAH AFUNGUA AKAUNTI MPYA HUKO ENGLAND

admin August 10, 2019 12:59 pm


MOHAMED Salah, mshambuliaji wa Liverpool ameanza kwa kasi msimu mpya wa Ligi Kuu England 2019/20.

Salah raia wa Misri anayekipiga pia kwenye timu ya Taifa amefungua akaunti mpya ya kupachika mabao ndani ya Ligi Kuu England.

Mechi ya kwanza iliyochezwa Jana Ijumaa Uwanja wa Anflied, Liverpool iliwanyoosha mabao 4-1 wapinzani wao Norwich City.

Salah alifungua akaunti yake dakika ya 19 akimalizia pasi ya Robert Firmino.

Huu ni mwanzo mzuri kwa nyota huyo ambaye msimu uliopita aliibuka mfungaji bora ndani ya Ligi Kuu England baada ya kupachika jumla ya mabao 22.

KIKOSI CHA SIMBA KITAKACHOANZA LEO DHIDI YA UD do SONGO KIKOSI CHA YANGA LEO KIMATAIFA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply