Uncategorized

YONDANI ALIPWA NUSU YA FEDHA ZAKE LAKINI ……

admin August 13, 2019 8:59 am


Wakati Andrew Vincent na Juma Abdul wakiwa wanadai jumla ya milioni 58, beki Kelvin Yondani amelipwa nusu ya fedha zake.

Yondani amelipwa milioni 15 kati ya 25 ambazo alikuwa akidai na sasa amebakiza deni la milioni 10.

Yondani naye ni mmoja wa wachezaji ambao hawakuwa kambini Yanga pamoja na wawili tajwa hapo juu kutokana na kutolipwa fedha hizo.

Mabosi wa Yanga wamekuwa wakipambana kusaka fedha ili kulipa fedha za wachezaji wao ambapo hivi sasa zoezi la kuichangia timu limekuwa likiendelea kupitia kwa wanachama wake.

Hivi sasa Yanga iko katika maandalizi ya kucheza mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Township Rollers ambapo kikosi kimeondoka Dar es Salaam kuelekea nyanda za kaskazini kuweka kambi maalum kuelekea mechi hiyo.

WAWILI WADAI MILIONI 58 YANGA BEKI MPYA SIMBA AJA NA KITISHO YANGA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply