Uncategorized

BALINYA AMWAGIWA NOTI ZA MAANA YANGA, MIFEDHA MINGINE KUTOLEWA

admin August 26, 2019 11:12 am


Straika wa Yanga, Juma Balinya, juzi alimwagiwa noti za maana na mashabiki wa timu hiyo wanaoishi Bostwana.

Fedha hizo zilitokana na kufunga bao muhimu ambalo liliipa nafasi Yanga ya kuendelea kusalia kunako Ligi ya Mabingwa Afrika.

Balinya aliifungia Yanga bao mnamo dakika ya 42 katika mechi ambayo ilimalizika kwa ushindi wa 1-0 na kuiwezesha kukutana na Zesco United katika mchezo utakaofuata.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Yanga, Mshindo Msolla, amethibitisha ni kweli Balinya alipokea fedha hizo kutoka kwa mashabiki.

Aidha, Msolla, ameeleza kuwa wamepanga kuwapa fedha wachezaji wote waliokuwa kwenye msafara kama motisha na yote hii inachagizwa na ushindi wa juzi.

MWINYI ZAHERA AVURUGWA YANGA MWIGULU: NILIJUA YANGA WATAIFUNGA ROLLERS

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply