Uncategorized

YANGA YACHOMOLEWA BETRI MOJA BILA KWA YAI RUVU SHOOTING WAKIFUTA UTEJA DAR

admin August 28, 2019 3:22 pm


Na George Mganga

Dakika 90 zimemalizika katika Uwanja wa Taifa kwa Yanga kupokea kichapo cha bao 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu Bara kwa timu hizo mbili.

Bao pekee na Ruvu Shooting limewekwa kimiani na Sadat Mohammed akimvisha kanzu kipa Farouk Shikalo mnamo dakika ya 20 kipindi cha kwanza.

Bao hilo limeweza kudumu kwa dakika zote 90 mpaka Mwamuzi Martin Saanya alipohitimisha mchezo wa kupuliza kipyenga cha mwisho, ubao ukisomeka 1-0.

Katika mechi hiyo, Kocha Mwinyi Zahera aliwatoa wachezaji Sadney Urikhob na kumwingiza Maybin Kalengo, Juma Balinya akimtoa pia na nafasi yake akichukua Balama Mapinduzi lakini mabadiliko hayakuleta mafanikio.

Ruvu imeweka rekodi kwa mara ya kwanza kufuta uteja kwa Yanga tena ikiibuka mshindi ikiwa ugenini.

Kama mdau wa michezo, unaweza kutuambia Yanga waliteleza wapi? Ndondosha maoni yako hapo chini.


LIVE! YANGA VS RUVU SHOOTING, LIGI KUU VODACOM RUVU SHOOTING YAFICHUA KILICHO NYUMA YA USHINDI WAO LEO MBELE YA YANGA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply