Uncategorized
MTIBWA SUGAR WAIPA TANO SAHARE STARS
admin
January 30, 2020
10:22 am
KOCHA Mkuu wa Mtibwa Sugar, Zuber Katwila amesema kuwa timu ya Sahare Stars ipo vizuri na ikipambana itafikia malengo iliyojiwekea.
Sahare iliwanyoosha Mtibwa Sugar kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho hatua ya 32 bora kwa kuwaondoa kwenye reli vigogo hao wanaoshiriki Ligi Kuu Bara kwa ushindi wa penalti 3-2 baada ya kutoshana nguvu ya kufungana bao 1-1 ndani ya dakika 90.
Katwila amesema kuwa walicheza vizuri na walionyesha ushindani jambo lililowapa nafasi ya kusonga mbele.
“Tulikuwa na changamoto kutoka kwao na ushindani ulikuwa mkubwa. Tumetolewa kwa penalti tumekubali kushindwa kwani tulikuwa nyumbani na mpira umechezwa wanastahili pongezi nasi tunajipanga kwa ajili ya mechi zetu nyingine zinazofuata,” alisema.
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.