Uncategorized

JOSE MOURINHO AANZA MIKWARA YAKE KWA NYOTA WAKE MPYA SASA

admin February 4, 2020 3:09 pm


JOSE Mourinho, Kocha Mkuu wa Spurs amesema kuwa anaamini nyota wake mpya Steven Bergwijn ataonyesha makubwa mbele ndani ya timu yake.

Raia huyo wa Netherlands aliyekuwa akikipiga PSV Eindhoven alifunga bao lake la kwanza akiwa na timu yake ya Spurs mbele ya Manchester City kwenye mchezo wa Ligi Kuu England.

Mourinho amesema kuwa hakuna haja ya kujiuliza maswali mengi juu ya kijana huyo ana amini ataonyesha kazi kubwa ndani ya Uwanja.

Bao la kwanza alifunga Bergwijin dakika ya 63 na la pili lilifungwa na Son Heung-Min dakika ya 71 na kuwafanya Spurs kufikisha jumla ya pointi 37 nafasi ya tano huku City wakiwa na pointi 51 nafasi ya pili.

KUMBE NAMUNGO INABEBWA NA HIKI HAPA BONGO NYOTA MPYA WA MANCHESTER UNITED APEWA MUDA WA MWEZI MMOJA NA KOCHA WAKE

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply