Uncategorized

UNITED WAONGEZEWA MZIGO KUINASA SAINI YA NAHODHA WA MBWANA SAMATTA

admin February 9, 2020 6:14 pm

MANCHESTER United imeonyesha nia ya dhati ya kuipata saini ya nyota wa Aston Villa, Jack Grealish ili kuongeza nguvu dani ya kikosi hicho kwenye kipindi cha usajili majira ya joto.
Grealish ambaye ni nahodha wa Mbwana Samatta amewekwa kwenye hesabu za kutua United kutokana na kuumia kwa nyota wao Marcus Rashford ambaye atakaa nje ya uwanja kwa muda wa miezi sita.
Kwenye Ligi Kuu England, Grealish ametupia mabao saba na pasi tano za mabao jambo linaloifanya United kumuweka namba moja kwa nyota ambao wanawaniwa.
 Kiungo huyo mwenye miaka 24 hakuwa na mpango wa kusepa ndani ya mwezi Januari kwenye klabu hiyo lengo lake lilikuwa ni kuona anatimiza majukumu ndani ya klabu yake anayoipenda kwa kufanya vizuri kwenye ligi pamoja na Kombe la Carabao.
Barcelona na Real Madrid nao pia wameongeza uzito kwenye mchakato wa kinasa saini ya nyota huyo.
KUTANA NA BILIONEA WA MISRI BOSI WA SAMATTA, ANAYEIMILIKI ASTON VILLA WAAMUZI WAJITOA LIGI KUU BARA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply