Uncategorized

MEDDIE KAGERE ATAJA SABABU INAYOMPONZA ASHINDWE KUFUNGA KWENYE BAADHI YA MECHI BONGO

admin February 25, 2020 4:14 am


MEDDIE Kagere, mshambuliaji wa Simba ambaye ni kinara wa kutupia ndani ya ligi amesema kuwa sababu kubwa iliyokuwa ikimfanya ashindwe kufunga kwenye mechi za hivi karibuni ni kubanwa na mabeki muda wote.

Kagere ametupia mabao 14 kati ya 50 yaliyofungwa na Simba, hakufurukuta kwenye baadhi ya mechi ambazo Simba ilicheza mfululizo.

Mechi hizo ilikuwa dhidi ya JKT Tanzania, Uwanja wa Uhuru Simba ilichapwa bao 1-0, Mtibwa 0-3 Simba, Lipuli 0-1 Simba, alikuja kuibukia mbele ya Kagera Sugar alifunga kwa penalti na mchezo wao dhidi ya Biashara United alifunga pia.

Kagere amesema:-“Nimekuwa nikipambana kwa ajili ya timu na wachezaji wenzangu, wote tunashirikiana na kufanya kazi tukiwa ni timu, kinachonifanya kwenye baadhi ya mechi kutofunga ni mabeki wengi kunitazama na kunifuatilia muda wote”.

EDEN HAZARD MAJANGA JUU YA MAJANGA HUKO REAL MADRID SADIO MANE APELEKA MAUMIVU KWA WESTHAM UNITED, LIVERPOOL BALAA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply