Uncategorized

KOCHA STARS: TEKNOLOJIA MPYA ITANIRAHISISHIA KAZI

admin March 17, 2020 5:12 am


KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Etienne Ndayiragije amesema kuwa teknolojia mpya inayotumika ndani ya timu hiyo kwa sasa itamrahisishia kazi ya kutambua muda na uwezo wa wachezaji wake wakiwa  kwenye mazoezi.

Ndayiragije amesema kuwa kwa sasa wachezaji wanatumia vifaa maalumu ambavyo wanavivaa (GPS) wakiwa mazoezini vitasaidia kutambua utimamu wa mwili kwa wachezaji.

“Vifaa wanavyovaa wachezaji wakiwa mazoezini vinasaidia kutambua utimamu wa mwili pamoja na uwezo wao na muda ambao wamefanya mazoezi hiyo inarahissha katika kutambua ubora wao.

“Hivi pia vimekuwa vikitumiwa na wachezaji wakubwa katika kufanya kwao mazoezi ni kitu kizuri na nina imani kitakuwa na matokeo chanya,” amesema.

MTIBWA SUGAR KESHO KUMALIZANA NA COASTAL UNION UONGOZI WA YANGA WAKANUSHA ISHU YA KUMTUHUMU MKUU WA MKOA WA DAR

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply