Uncategorized
MANCHESTER UNITED YAINGIA ANGA ZA BARCELONA, WAITAKA SAINI YA BEKI WA KATI UMTITI
SAMUEL Umtiti, beki wa kati wa Barcelona yupo kwenye hesabu za kusajiliwa na klabu ya Manchester United.
Nyota huyo anatarajiwa kusajiliwa ndani ya United kwenye usajili ujao wa kipindi cha joto.
Umtiti mwenye miaka 26 yupo katikati ya msimu wake ndani ya Camp Nou lakini hana uhakika wa nafasi ya kuanza ndani ya kikosi cha kwanza.
United inaonekana ipo mstari wa mbele kuinasa saini ya beki huyo anayetumia mguu wa kushoto na Kocha Mkuu wa Barcelona, Quique Setien yupo tayari kumuachia.

Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.