Uncategorized

KUMBE KOCHA WA YANGA ALITAKA KUJA BONGO MIAKA MINNE ILIYOPITA

admin March 20, 2020 4:31 am


KOCHA Mkuu wa Yanga, Luc Eymael,amesema kuwa alikuwa ana mpango wa kuja Bongo miaka minne iliyopita lakini mambo hayakuwa kama alivyotarajia akabaki Afrika Kusini. 

Kwa sasa Eymael anakiongoza kikosi cha Yanga ambacho kinashiriki Ligi Kuu Bara akipokea kijiti cha aliyekuwa Kocha Mkuu, Mwinyi Zahera ambaye alipigwa chini kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni mwenendo mbovu wa timu.

Eymael amesema :”Nilikuwa nina mpango wa kuja Bongo miaka minne iliyopita kuifundisha Yanga, sababu kubwa nilikuwa napenda kuja Tanzana ila mambo hayakwenda sawa.

“Kwa sasa nipo ndani ya Yanga ninaendelea na maisha na kuna mengi ambayo ninayafanya ila yote kwa yote ninafurahi kuwa Tanzania,” amesema Eymael.

MUONEKANO WA UKURASA WA NYUMA GAZETI LA CHAMPIONI IJUMAA SHEVA APEWA MAZOEZI MAALUMU, AWAOMBA MASHABIKI WAMUOMBEE

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply