Uncategorized

WAWILI WAJIENGUA NDANI YA YANGA KWENYE NAFASI ZAO ZA UONGOZI

admin March 27, 2020 2:57 pm


 SHIJA Richard, Mjume wa Kamati ya Yanga inaelezwa kuwa amejiuzulu nafasi hiyo leo Machi 27 bila kuweka wazi sababu za kujiuzulu kwake.


Richard ni miongoni mwa wajumbe watatu wanaotuhumiwa kutokuwa na mahusiano mazuri na Kampuni ya GSM ambayo hivi karibuni ilitangaza kubakia kuwa mdhamini kama mkataba wake unavyoelekeza.

 Richard amedai kuwa klabu hiyo ni kubwa kuliko mtu hivyo ameamua kujiweka pembeni. 


“Nimeamua kwa hiari yangu kujiuzulu nafasi zote za uongozi katika klabu yangu ya Yanga ambayo ni kubwa kuliko mimi na kuliko mtu yeyote.

 “Ukweli hata usipousema, huwa una tabia ya kujitokeza wenyewe japo taratibu lakini huwa unadumu milele,” imeeleza taarifa hiyo.

Mjumbe mwingine ambaye amejieungua ni pamoja na Rodgers Gumbo ambaye naye inaelezwa kuwa amejiengua.

Alipotafutwa Ofisa Habari wa Yanga, Hassan Bumbuli ili azungumzie suala hili hakuwa tayari.

MUUAJI WA SIMBA AJICHIMBIA DODOMA KUNOA KIWANGO CHAKE LUSAJO AFUNGUKA ISHU YAKE YA KUTUA YANGA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply