Uncategorized

KMC WAPIGA MATIZI YAO BINAFSI, HIVI NDIVYO WANAVYOFUATILIWA

admin April 11, 2020 2:06 pm


UONGOZI wa KMC umesema kuwa kwa sasa wachezaji wote wamepewa program ya kufanya wakiwa kwenye mapumziko kupisha maambukizi ya Virusi vya Corona.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa KMC, Anwar Binde amesema kuwa wamekuwa wakiwafuatilia wachezaji wao kupitia mitandao ili kujua namna gani wanaendelea na mazoezi.

“Wachezaji wapo nyumbani kwa sasa wakiendelea na mazoezi binafsi ambayo wamepewa na benchi la ufundi.

“Ni ngumu kujua kwamba kwa namna gani wanaendelea ila tunashukuru Mungu kwa kuwa tunawaona kupita makundi yetu na hii inatupa nguvu ya kuamini kwamba wanafanya kile wanachoelekezwa pia tumewaambia wachukue tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona,” amesema.

ISHU YA CHAMA KUTUA YANGA IMEFIKIA HAPA AKITUA HUYU JANGWANI, ENEO LA KATI VITA YA NAMBA ITAKUWA SI MCHEZO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply