Uncategorized

JONAS MKUDE HATAKI MCHEZO NDANI YA SIMBA

admin April 12, 2020 12:36 pm
JONAS Mkude, kiungo wa Simba amesema kuwa kwa sasa anajifua vilivyo ili kulinda kipaji chake alichonacho.

Kwa sasa Ligi Kuu Bara imesimama kupisha maambukizi ya Virusi vya Corona wachezaji wengi wapo nyumbani baada ya kambi kuvunjwa.

Mkude amesema:”Kwa sasa ninafuata maelekezo niliyopewa na Kocha Mkuu (Sven Vandenbroek) ili kuwa fiti na ninachukua pia tahadhari kuhusu Virusi vya Corona.

“Kocha ametoa program maalumu ambayo ninaifanyia kazi na ni muhimu kufanya hivyo ili kuwa bora kwani mazoezi ni muhimu,” .

Mkude amehusika kwenye mabao manne ambapo amefunga mawili na kutoa pasi mbili huku Simba ikiwa imefunga mabao 63.
MKUDE – KWA SASA SITAKI UJINGA UJINGA..!! LAUTARO MARTINEZ AZIVURUGA KLABU ZA ENGLAND, LA LIGA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply