Uncategorized

MNATA ATAJA ANACHOKIPATA KUTOKA KWA SHIKALO

admin April 16, 2020 11:31 am


METACHA Mnata, mlinda mlango namba mbili wa Yanga amesema kuwa anakubali uwezo wa mlinda mlango namba moja wa Yanga, Farouk Shikalo kutokana na kuwa na vitu tofauti.

Shikalo raia wa Kenya ni mlinda mlango namba moja huku namba mbili akiwa ni Mnata ambaye ni mzawa.

Mnata amesema:”Nimekuwa nikijifunza mengi kupitia kwa Shikalo ambaye ni kipa mwenzangu ndani ya Yanga, jambo hilo linanifanya nami nizidi kujifunza bila kuchoka.

“Ukiwa mlinda mlango una kazi kubwa ya kuokoa na kujifunza pale ambapo unakuwa upo benchi hivyo wakati ule ligi ilipokuwa inaendelea nilikuwa ninajifunza mengi,”.

Kwa sasa Ligi Kuu Bara imesimama kupisha maambukizi ya Virusi vya Corona ambavyo vimesababisha ligi nyingi duniani kusimamishwa.


BERNARD MORRISON;MAMBO YANGEKUWA SAWA, NINGESAINI SIMBA VIDEO: NAMNA YANGA ILIVYOJADILIWA BUNGENI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply