Uncategorized

BEKI WA COASTAL UNION AZIPASUA KICHWA SIMBA NA YANGA

admin April 22, 2020 2:05 pm


BAKARI Mwamnyeto, beki wa Coastal Union ameziingiza vitani timu za Kariakoo, Simba na Yanga ambazo zote zinaisaka saini yake.

Mwamnyeto amekuwa kwenye hesabu kali na mabosi wa Simba ambao wanahitaji kuongeza nguvu kikosini hapo kwa ajili ya msimu ujao.

Habari zinaeleza kuwa tayari mabosi wa Yanga wameingia kwenye mpango wa kuinasa saini yake ili kumuongezea nguvu Lamine Moro na Kelvin Yondani.

Mussa Kassa, meneja wa beki huyo amesema kuwa amepata dili nyingi zinazomtaka beki huyo ikiwa ni pamoja na Simba na Yanga.

“Simba na Yanga wamekuwa kwenye mpango wa kumpata beki wa Coastal Union ila nimewaambia kwamba ikiwa wapo siriaz wazungumze na Coastal Union ambao wao ndio mchezaji wao kwa sasa.

“Kuhusu gharama za mchezaji na dau lake siwezi kuliweka mezani kwa sasa kwani ni suala la makubaliano,” amesema.

BEKI RUVU SHOOTING AJIWEKA SOKONI KISA NKANA…WAZAMBIA WAMCHANA CHAMA KUWA SI MZALENDO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply