Uncategorized

YANGA YAWAOMBA MASHABIKI KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA CORONA

admin April 27, 2020 12:02 pm


BERNARD Morrison, kiungo mshambuliaji wa Yanga amewaomba mashabiki kuendelea kufanya dua ili hali irejee kama zamani.

Kwa sasa Ligi Kuu Tanzania Bara imesimama kutokana na maambukizi ya Virusi vya Corona ambavyo vinaitikisa dunia.

Wakati Ligi Kuu Bara inasimamishwa na Serikali Machi 17 Yanga ilikuwa nafasi ya tatu ikiwa na pointi 51 baada ya kucheza mechi 27.

Morrison amesema:-“Tuendelee kumuomba Mungu maisha ya kawaida yarejee baada ya hili janga la Corona na turudi kufanya kazi ili mashabiki na wapenda soka wafurahie kazi yetu.

“Kwa sasa ninachukua tahadhari nikiwa nyumbani pia ninapeda kuona mashabiki pia wakichukua tahadhari kwani janga hili lipo na Virusi ni hatari,” .

MTUPIAJI NAMBA MOJA MBAO KUSEPA NGOMA BADO NGOMA NZITO AZAM FC

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply