Uncategorized

YANGA YAWAOMBA MASHABIKI KULIPOKEA JARIDA LAO, KUNA BONGE LA OFA

admin May 3, 2020 4:13 pm

UONGOZI wa Yanga umewaomba mashabiki na wanachama wa klabu hiyo kulipokea Jarida la Yanga kwa kununua zaidi nakala.

Yanga hivi karibuni ilizindua jarida hilo ambalo linahusu masuala muhimu ya Yanga kwa ajili ya kuwahabarisha mashabiki na wanachama wake.

Ofisa Uhamasishaji wa Yanga, Antonio Nugaz amesema:-“Moja ya jambo muhimu kwa wanachama, wapenzi na mashabiki wa Yanga SC ni kulipokea jarida kwa kununua nakala.

“Unaweza kupata jarida letu kwenye maduka yote ya GSM kwa Sh 5,000 au nunua jezi kwa Sh 20,000 upate jarida bure, Makao Makuu ya Klabu ya Yanga, Matawi ya Yanga nchi nzima.”

VIDEO: KISA CORONA, OFISA HABARI WA SIMBA ATOA KAULI TSHABALALA YEYE MABAO YAKE NI MBELE YA WAKATA MIWA TU, SIRI YAKE HII HAPA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply