Uncategorized

NYOTA YANGA AMKARIBISHA MSHAMBULIAJI WA SIMBA KIKOSINI

admin May 13, 2020 5:11 am
MARCEL Kaheza mshambuliaji wa Polisi Tanzania anayekipiga kwa mkopo akitokea Klabu ya Simba amesema kuwa mshikaji wake Ditram Nchimbi anayekipiga ndani ya Yanga amemkaribisha kikosini humo.

Kaheza mkataba wake na Simba unameguka msimu huu utakapokamilika hivyo atakuwa mchezaji huru iwapo Simba hawatamuongezea dili jingine.

Pacha yake na Nchimbi ndani ya PolisiTanzania ilianza kujibu ambapo kwenye sare ya kufungana mabao 3-3 dhidi ya Yanga alimtengenezea pasi mbili za mabao Nchimbi ambaye alikuwa akicheza Polisi Tanzania na sasa yupo zake Yanga. “Nimekuwa nikiwasiliana na Nchimbi kwani sisi ni marafiki kwa muda mrefu, tulifanikiwa  kutengeneza pacha nzuri ndani ya Polisi Tanzania. “Nchimbi amekuwa akiniambia nipambane niwe bora muda wote ikiwezekana nipate dili la kuibukia Yanga ili tukiwashe tena pamoja,” amesema.

Kaheza ametupia mabao saba ndani ya Polisi  Tanzania iliyo chini ya Kocha Mkuu,  Malale Hamsini.

MSHAMBULIAJI WA ORLANDO PIRATES AKUBALI KUTUA SIMBA MATUMAINI YAMEANZA KUONEKANA LIGI KUREJEA ILA KUNA UMUHIMU WA KUANZA MAANDALIZI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply