Uncategorized

SIMBA YATAKA KUBEBA MATAJI MAKUBWA MAWILI

admin May 23, 2020 11:47 am

MTENDAJI Mkuu wa Simba, Senzo Mbatha amesema kuwa mpango mkubwa uliopo kwa timu hiyo ni kupambana kupata mataji makubwa mawili msimu huu wa 2019/20.

Mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Bara leo walikuwa wanazindua mpango kazi wa kusambaza taarifa mtandaoni ambao ni tovuti itakayorahisisha kazi ya kutoa taarifa.

Senzo amesema:”Lazima tujikite kuhakikisha tunashinda ligi kuu na FA. Hiyo ndio dhamira yetu kwa sasa.”

Kombe la FA Simba imetinga robo fainali huku kwa upande wa Ligi Kuu Bara ikiwa nafasi ya kwanza na pointi 71 baada ya kucheza mechi 28.

TARIMO AWASHUKURU WATANZANIA AWAOMBA WAMFUATE INSTAGRAM TIMO WERNER AZICHANGANYA LIVERPOOL NA CHELSEA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply