Uncategorized

HAALAD ASHAURIWA KUIBUKA NDANI YA LIVERPOOL

admin June 12, 2020 6:47 am


ERLING Haaland, mshambuliaji mwenye miaka 19 anayekipiga ndani ya Klabu ya Borussia Dortmund inayoshiriki Bundesliga nchini Ujerumani anatajwa kuwa kwenye rada za Manchester United na Liverpool ambao wanahitaji saini yake.

Mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa ya Norway, Jan Age Fjortof amesema kuwa sehemu bora itakayomfaa mshambuliaji huyo ni Liverpool na sio Manchester United.


Jan amesema kuwa uwezo wa mshambuliaji huyo anaweza kufiti Kwenye kikosi chochote duniani lakini sehemu pekee itakayomfaa ni Liverpool.


Haaland amekuwa akiwindwa na timu nyingi za Ligi Kuu England hivyo kubaki ndani ya Bundesliga msimu ujao nafasi inaonekana kuwa ndogo.


 “Ni mchezaji mzuri anaweza kucheza popote ila Liverpool ni bora kwake,” amesema.

EYMAEL, MOLINGA NA OFISA UHAMASISHAJI WAIFUATA MWADUI LEO MKUDE KUIKOSA RUVU SHOOTING TAIFA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply