Uncategorized

SIMBA:ITAKUWA KAZI NGUMU MBELE YA MWADUI FC ILA TUPO TAYARI

admin June 19, 2020 6:47 am


UONGOZI wa Simba umesema kuwa upo tayari kwa mchezo wa kesho dhidi ya Mwadui FC utakaochezwa Uwanja wa Taifa majira ya saa 10:00 jioni.

Akizungumza na Saleh Jembe, Meneja Mkuu wa Simba, Patrick Rweyemamu amesema kuwa wapo tayari kwa kusaka pointi tatu mbele ya Mwadui.

“Mchezo wetu uliopita mbele yao tulipoteza hivyo nasi pia tumejipanga kuona namna gani tutapata pointi tatu mbele ya Mwadui FC.

“Utakuwa mchezo mgumu ila tupo tayari kwa ajili ya kupambana na maandalizi yapo sawa kwani wachezaji wapo tayari,” amesema.

Bao pekee la ushindi kwa Mwadui FC lilifungwa na Gerald Mdamu ambaye ana mabao matano na pasi tatu za mabao.

LEO LIGI DARAJA LA KWANZA MAMBO YANAANZA ISHU YA KUFUNGIWA MASHABIKI JKT TANZANIA WAOMBA MSAMAHA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply